1. Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika usiku wa Cheo na Utukufu.

Rudi kwenye Sura

2. Na kitu gani kitakufunza ni nini usiku huo wa Cheo na Utukufu?

Rudi kwenye Sura

3. Usiku wa Qadr na Sharaf, Cheo na Utukufu,  ni bora kuliko miezi elfu, kwa kuwa umekhusika kwa kuteremka ndani yake Qur'ani tukufu.

Rudi kwenye Sura

4. Huteremka Malaika na Jibrili katika usiku huo mpaka kwenye ardhi kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa sababu ya kila jambo.

Rudi kwenye Sura

5. Na wameaminika na maudhi na uovu. Hali inabaki  hivyo mpaka mapambazuko ya alfajiri.

Rudi kwenye Sura