1. Naapa kwa mwangaza wa asubuhi unapo ufukuza usiku.

Rudi kwenye Sura

2. Na kwa masiku kumi yaliyo tukuzwa na Mwenyezi Mungu. (Na hayo ni masiku kumi ya mwanzo wa Mwezi wa Alhaj, Mfungo Tatu).

Rudi kwenye Sura

3. Na shafi' yaani hisabu inayo gawika kwa mbili, kama 4, 6, 8 n.k. na witri, yaani isiyo gawika kwa mbili, kama 1, 3, 5 n.k. katika kila kitu.

Rudi kwenye Sura

4. Na kwa usiku unapo pita kwa kwenda ulimwengu kwa namna ya ajabu.

Rudi kwenye Sura

5. Je! Katika vitu vilivyo tajwa vinavyo onekana kwa akili hapana kiapo cha kukinaisha?

Rudi kwenye Sura

6,7. Kwani hujui jinsi Mola wako Mlezi alivyo wateremshia adhabu yake kaumu ya Hud, watu wa Iram wenye majengo marefu?

Rudi kwenye Sura

8. Ambayo haikupata kujengwa mfano wake kwa umadhubuti na ujenzi katika nchi.

Rudi kwenye Sura

9. Kwani hukujua jinsi Mola wako Mlezi alivyo teremsha adhabu yake kwa Thamudi, kaumu ya Saleh, walio chonga majabali kujengea nyumba zao huko bondeni?

Rudi kwenye Sura

10. Au kwani hukujua vipi Mola wako Mlezi alivyo wateremshia adhabu yake Firauni mwenye majeshi yaliyo upa nguvu ufalme wake kama vigingi vinavyo simamisha makhema?

Rudi kwenye Sura

11. Ambao walipita mipaka katika nchi?

Rudi kwenye Sura

12. Na wakazidisha kufanya uharibifu kwa ukafiri na udhalimu?

Rudi kwenye Sura

13. Basi Mola wako Mlezi aliwateremshia adhabu kali ya kuwaunguza.

Rudi kwenye Sura

14. Hakika Mola wako Mlezi anaviangalia vitendo vya watu, na anawahisabia, na atakuja kuwalipa kwavyo.

Rudi kwenye Sura

15. Ama mtu akijaribiwa na Mola wake Mlezi na akamkirimu, na akamneemesha kwa mali na cheo na nguvu, basi husema kwa kughurika na hayo: Mola wangu Mlezi amenitukuza kwa kuwa ninastahiki haya!

Rudi kwenye Sura

16. Na pindi Mola wake Mlezi akimjaribu mtu kwa kumdhikisha riziki, basi hughafilika na hikima ya hayo na husema: Mola wangu Mlezi kanidhalilisha!

Rudi kwenye Sura

17. Wacheni mtindo huo! Mambo siyo hayo kama msemavyo; bali nyinyi hamumkirimu yatima;

Rudi kwenye Sura

18. Wala hamhimizani kuwalisha masikini;

Rudi kwenye Sura

19. Na mnakula mali ya urithi kwa pupa, hamchagui linalo faa na lisilo faa.

Rudi kwenye Sura

20. Na mnayapenda mali mno, yanayo kupelekeeni kupapatika katika kuyakusanya na ubakhili wa kuyatumia.

Rudi kwenye Sura

21. Wacheni vitendo hivyo! Kwani inakungojeeni siku itapo lazwa ardhi iwe sawa sawa,

Rudi kwenye Sura

22. Na aje Mola wako Mlezi kama anavyo stahiki kuja kwake Subhanahu na Malaika waje kwa safu safu;

Rudi kwenye Sura

23. Na siku hiyo iletwe Jahannamu, nyumba ya adhabu,  siku hiyo yatapo tokea hayo mwanaadamu atakumbuka aliyo yaharibu - lakini wapi! Kukumbuka huko kumfae nini, na wakati umekwisha pita?

Rudi kwenye Sura

24. Atasema kwa majuto: Laiti ningeli jitangulizia katika dunia vitendo vyema vya kunifaa katika maisha ya Akhera!

Rudi kwenye Sura

25,26. Siku hiyo zitakuwa hali hizi, haadhibu mtu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala hafungi mtu kama afungavyo Yeye.

Rudi kwenye Sura

27. Ewe nafsi uliye tulia juu ya Haki!

Rudi kwenye Sura

28. Rejea kwenye radhi ya Mola wako Mlezi nawe uradhi kwa neema ulio pewa, nawe umemridhisha kwa a'mali uliyo ikadimisha.

Rudi kwenye Sura

29. Basi ingia katika kundi la waja wangu walio wema!

Rudi kwenye Sura

30. Na ingia katika Pepo yangu, nyumba ya neema ya milele!

Rudi kwenye Sura