112 SUURATUL IKHLAS

Sura hii imeteremshwa Makka, na ina Aya 4

Kwa jina la Mwenyeezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

1. Sema: Yeye Mwenyeezi Mungu ni Mmoja.

2. Mwenyeezi Mungu ndiye anayekusudiwa kwa haja.

3. Hakuzaa wala hakuzaliwa.

4. Wala hana anayefanana naye hata mmoja.[1]


[1] Aya 3-4

MUNGU N1 MMOJA TU

Iliposemwa: "Hakuzaa" Yaani, Hakuzaa kama alivyozaa Mariam. "Wala hakuzaliwa" Yaani. Hakuzaliwa kama alivyozaliwa Issa (Yesu).

Tutaangalia somo hili kwa mujibu wa vitabu vya Wakristo kama ifuatavyo:

"Kwa kuwa ndiye uliye mkuu, wewe ndiwe mfanya miujiza ndiwe Mungu peke yako." Zaburi 86:10.

 "Naye Hezekia akaomba mbele za Bwana, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia, wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi." 2 Wafalme 19:15.

"Mwawezaje kuamini ninyi mnaopokeana utukufu ninyi kwa ninyi, na utukufu ule utokao kwa Mungu aliye wapekee hawamtafuti? Yohane 5:44.

"Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli,

na Yesu Krsito uliyemtuma." Yohane 17:3.

"Basi kwa habari ya kuvila vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, twajua ya kuwa sanamu si kitu katika ulimwengu, na ya kuwa hakuna Mungu ila mmoja tu. Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi, lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu." 1 Wakorintho 8:4-6.

Bwana, Mfalme wa Israeli, asema hivi: "Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho, zaidi yangu mimi hapana Mungu." Isaya 44:6.

"Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine, zaidi yangu mimi hapana Mungu."

Isaya 45:5.

"Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine." Isaya 45:18.

"Bwana asema hivi; iko wapi hati ya talaka ya mama yenu, ambayo kwa hiyo naliachana naye?" Isaya 50:1.

SIFA ZA MUNGU

"Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu, maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu." Yakobo 1:13.

Lakini Yesu alijaribiwa na Iblisi:

Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Iblisi." Mathayo 4:1.

"Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote ya ufalme wangu watetemeke na kuogopa mbele za Mungu wa Danieli, maana yeye ndiye Mungu aliye hai, adumuye milele. Na ufalme wake ni ufalme usioharibika, na mamlaka yake itatudumu hata mwisho." Danieli 6:26.

Lakini Yesu akafa:

"Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake," Mathayo 27:50.

"Basi, usikie huko mbinguni, makao yako, akasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake, wewe ujuaye moyo wake maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote." 1 Wafalme 8:39.

Lakini Yesu hakujua kila kitu:

"Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa, akaona mti mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu." Mathayo 21:18.

Je, wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki, akili zake hazichunguziki." Isaya 40:28.

Lakini Yesu alichoka:

"Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani." Yohane 4:6.

YESU N1 MTUME

Mtume, katika Kiyunani ni: Apostolos. Yaani, Aliyetumwa.

"Maana MUNGU hakumtuma. Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye." Yohane 3:17.

"Yesu akawaambia, chakula changu ndicho hiki: Niyatende mapenzi yake aliyonipeleka, nikaimalize kazi yake." Yohane 4:34.

"Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe, kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo, na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyonipeleka." Yohane 5:30.

"Lakini ushuhuda nilio nao mimi ni mkubwa kuliko ule wa Yohane, kwa kuwa zile kazi alizonipa Baba ili nizimalize, kazi hizo zenyewe ninazozitenda, zanishuhudia ya kwamba Baba amenituma." Yohane 5:36.

"Yesu akawaambia, kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja, wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma. Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo?" Yohane 8:42.

"Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma." Yohane 17:3.

MWANA WA MUNGU

Maneno haya katika Biblia hayahusiki na Mwana halisi wa Mungu, bali humwelekea mtu ateuliwaye na kuchukuliwa na Mungu kama mwanae. Tutataja mifano michache hapa:

"Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana." Ayubu 1:6.

"Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi: Israeli ni mwanangu mimi mzaliwa wa kwanza wangu." Kutoka 4:22.

"Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu, msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa." Kumbukumbu 14:1.

YESU SI MWEMA

"Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamuuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu." Marko 10:17.

YESU HAKUFA MSALABANI

"Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu na kuwa amesulubiwa? Wagalatia 3:1.

"Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu, maana imeandikwa: Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti." Wagalatia 3:13.

"Mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti, lazimna utamzika siku hiyo hiyo, kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu." Kumbukumbu 21:23.

"Basi, usikie huko mbinguni, makao yako, akasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake, wewe ujuaye moyo wake rnaana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote." 1 Wafalme 8:39.

Lakini Yesu hakujua kila kitu:

"Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa, akaona mti mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila rnajani tu." Mathayo 21:18.

"Je, wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba

miisho ya dunia. hazimii. wala hachoki, akili zake hazichunguziki." Isaya

40:28

Lakini Yesu alichoka:

"Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani." Yohane 4:6.

YESU N1 MTUME

Mtume, katika Kiyunani ni: Apostolos. Yaani, Aliyetunrwa.

"Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu j-iokolewe katika yeye." Yohane 3:17.

"Yesu akawaambia, chakula changu ndicho hiki: Niyatende rnapenzi yake aliyonipeleka, nikaimalize kazi yake." Yohane 4:34.

"Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe, kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo, na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti rnapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyonipeleka." Yohane 5:30.

"Lakini ushuhuda nilio nao mimi ni mkubwa kuliko ule wa Yohane, kwa kuwa zile kazi alizonipa Baba ili nizimalize, kazi hizo zenyewe ninazozitenda, zanishuhudia ya kwamba Baba amenituma." Yohane 5:36.

"Yesu akawaambia, kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja, wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma. Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo?" Yohane 8:42.

"Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma." Yohane 17:3.

MWANA WA MUNGU

Maneno haya katika Biblia hayahusiki na Mwana halisi wa Mungu, bali

humwelekea mtu ateuliwaye na kuchukuliwa na Mungu kama mwanae. Tutataja mifano michache hapa:

"Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana." Ayubu 1:6.

"Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi: Israeli ni mwanangu mimi mzaliwa wa kwanza wangu." Kutoka 4:22.

"Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu, msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa." Kumbukumbu 14:1.

YESU SI MWEMA

"Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu rnmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamuuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele? Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu." Marko 10:17.

YESU HAKUFA MSALABANI

"Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu na kuwa amesulubiwa? Wagalatia 3:1.

"Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu, maana imeandikwa: Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti." Wagalatia 3:13.

"Mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti, lazima utamzika siku hiyo hiyo, kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu." Kumbukumbu 21:23.