109 SUURATUL KAAFIRUUN

Sura hii imeteremshwa Makka, na ina Aya 6

Kwa jina la Mwenyeezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

1. Sema: Enyi makafiri.

2. Siabudu mnachoabudu.

3. Wala nyinyi hamuabudu ninayemwabudu.

4. Wala sitaabudu mnachoabudu.

5. Wala nyinyi hamtaabudu ninayemwabudu.

6. Nyinyi mtapata malipo yenu nami nitapata malipo yangu.