103 SUURATUL A'SR

Sura hii imeteremshwa Makka, na ina Aya 3

Kwajina la Mwenyeezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

1. Naapa kwa alasiri.

2. Kwa hakika mwanadamu yumo hasarani.

3. Isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri, na wakausiana (kushikamana na) haki, na wakausiana kusubiri.