1. Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;

Rudi kwenye Sura

2. Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na cheo chake.

Rudi kwenye Sura

3. Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.

Rudi kwenye Sura

4. Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.

Rudi kwenye Sura

5. Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana awezae kumdhalilisha?

Rudi kwenye Sura

6. Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.

Rudi kwenye Sura

7. Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui yeyote hata huyo aliye muumba?

Rudi kwenye Sura

8,9. Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya kutazamia, na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?

Rudi kwenye Sura

10. Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?

Rudi kwenye Sura

11. Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi yake.

Rudi kwenye Sura

12. Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya milimani?

Rudi kwenye Sura

13. Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,

Rudi kwenye Sura

14. Au kumlisha siku ya njaa

Rudi kwenye Sura

15. Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.

Rudi kwenye Sura

16. Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.

Rudi kwenye Sura

17. Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.

Rudi kwenye Sura

18. Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa mkono wa kulia.

Rudi kwenye Sura

19. Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa kheri na watapata adhabu.

Rudi kwenye Sura

20. Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.

Rudi kwenye Sura