1. Jua litakapo kunjwa na mwangaza wake ukafutwa,

Rudi kwenye Sura

2. Na nyota ikazimwa nuru yao,

Rudi kwenye Sura

3. Na milima ikaondoshwa hapo ilipo,

Rudi kwenye Sura

4. Na ambao wa kuchukua mimba wakaharibu mimba zao,

Rudi kwenye Sura

5. Na nyama mwitu wakusanywe kutoka vichakani mwao na mashimoni mwao, hawajijui hawajitambui kwa wingi wa kufazaika.

Rudi kwenye Sura

6. Na bahari zikawa zinawaka moto,

Rudi kwenye Sura

7. Na roho zikaunganishwa na viwiliwili vyao,

Rudi kwenye Sura

8,9. Na mtoto wa kike aliye zikwa hai, akaulizwa kwa kumliwaza yeye, na kumshutumu aliye mzika hai, kwa makosa gani kauliwa, naye hana dhambi? (Ilikuwa ada ya makafiri wa Kiarabu kabla ya Uislamu kuwazika watoto wao wa kike nao wahai!  Baadhi ya Mabaniani wanawauwa watoto wao wa kike hata hivi leo huko India!!)

Rudi kwenye Sura

10. Na nyaraka zilizo andikwa ndani vitendo vya watu zikakunjuliwa wakati wa hisabu.

Rudi kwenye Sura

11. Na mbingu itapo ondoshwa pahala pake,

Rudi kwenye Sura

12. Na Moto ukawashwa kwa mwako mkali,

Rudi kwenye Sura

13. Na Pepo ikajongezwa ikawa karibu,

Rudi kwenye Sura

14. Yatakapo tokea yote hayo, basi hapo tena kila nafsi itajua nini iliyo tanguliza, ikiwa kheri au shari.

Rudi kwenye Sura

15. Naapa kiapo cha mkazo kwa nyota ambazo zinanywea zinapo chomoza, na hapo mwanga wake huwa khafifu,

Rudi kwenye Sura

16. Zenye kwenda na hujificha wakati wa kuchwa kwake, kama paa wanapo jificha kwenye mapango yao.

Rudi kwenye Sura

17. Na kwa usiku linapo pungua giza lake wakati unapo malizika.

Rudi kwenye Sura

18. Na kwa asubuhi unapo anza mwangaza wake na ukavuma upepo wake,

Rudi kwenye Sura

19. Hakika Qur'ani bila ya shaka ni kauli ya Mjumbe anaye toka kwa Mwenyezi Mungu, naye ni mwenye kuhishimiwa kwake,

Rudi kwenye Sura

20. Mwenye nguvu katika kutekeleza waajibu wake, mwenye cheo na daraja mbele ya Mwenyezi Mungu Mwenye Kiti cha Enzi.

Rudi kwenye Sura

21. Tena ni mwenye kut'iiwa, na muaminifu wa kuchukua wahyi miongoni wa walio juu.

Rudi kwenye Sura

22. Na huyo Mtume wenu ambaye ni mwenzenu, mnaye mjua kuwa ana akili timamu, si mwendawazimu.

Rudi kwenye Sura

23. Na ninaapa kuwa Muhammad s.a.w. bila ya shaka alimwona Jibrili katika upeo wa macho kwa mujibu wa inavyo onekana.

Rudi kwenye Sura

24. Na Muhammad si bakhili wa kufikisha wahyi na kuwafunza watu.

Rudi kwenye Sura

25. Wala huu wahyi (ufunuo) ulio teremshwa juu yake si kauli ya Shetani aliye fukuzwa kutoka kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu.

Rudi kwenye Sura

26. Basi njia gani iliyo ya uwongofu zaidi kuliko hii mnayo ifuata?

Rudi kwenye Sura

27. Qur'ani si chochote ila ni ukumbusho na mawaidha kwa walimwengu wote.

Rudi kwenye Sura

28. Kwa anaye taka, miongoni mwenu, kusimama sawa kufikilia haki na kweli.

Rudi kwenye Sura

29. Na nyinyi hamwezi kutaka kitu ila anapo taka Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Rudi kwenye Sura