1. Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,

Rudi kwenye Sura

2. Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.

Rudi kwenye Sura

3. Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,

Rudi kwenye Sura

4. Au atawaidhika na mawaidha yamfae.

Rudi kwenye Sura

5,6. Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake, wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.

Rudi kwenye Sura

7. Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?

Rudi kwenye Sura

8,9,10. Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu, naye anamkhofu Mwenyezi Mungu wewe unampuuza.

Rudi kwenye Sura

11. Hakika Aya hizi ni mawaidha.

Rudi kwenye Sura

12. Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.

Rudi kwenye Sura

13. Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,

Rudi kwenye Sura

14. Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.

Rudi kwenye Sura

15. Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;

Rudi kwenye Sura

16. Walio bora, wema.

Rudi kwenye Sura

17. Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?

Rudi kwenye Sura

18. Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?

Rudi kwenye Sura

19. Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye  Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.

Rudi kwenye Sura

20. Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.

Rudi kwenye Sura

21. Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.

Rudi kwenye Sura

22. Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.

Rudi kwenye Sura

23. Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.

Rudi kwenye Sura

24. Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!

Rudi kwenye Sura

25. Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.

Rudi kwenye Sura

26. Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.

Rudi kwenye Sura

27. Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.

Rudi kwenye Sura

28. Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.

Rudi kwenye Sura

29. Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,

Rudi kwenye Sura

30. Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,

Rudi kwenye Sura

31. Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).

Rudi kwenye Sura

32. Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.

Rudi kwenye Sura

33. Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,

Rudi kwenye Sura

34,35,36. Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake, na mama yake, na baba yake, na mkewe, na wanawe!

Rudi kwenye Sura

37. Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!

Rudi kwenye Sura

38,39. Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza, zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.

Rudi kwenye Sura

40. Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.

Rudi kwenye Sura

41. Zimegubikwa na kiza na weusi.

Rudi kwenye Sura

42. Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.

Rudi kwenye Sura