1. Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?

Rudi kwenye Sura

2,3. Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu, na wala hahimizi kulishwa masikini.

Rudi kwenye Sura

4,5. Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Sala zao wasinafiike nazo.

Rudi kwenye Sura

6. Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.

Rudi kwenye Sura

7. Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu.

Rudi kwenye Sura